Grumeti Fund

Grumeti Fund ni Shirika lisilo la faida linalochangia kuhifadhi Ikolojia ya
Serengeti kwa vizazi vijavyo.

TAZAMA VIDEO KAMILI

Kazi zetu

Sehemu nyingi ulimwenguni zinapoendelea kuharibika kutokana na ongezeko kubwa la watu, Grumeti Fund kwa kushirikiana na washirika wetu wa Tanzania inajizatiti katika kuhifadhi ekari 350,000 za eneo la Magharibi mwa Serengeti zilizopuuzwa hapo awali. Kupitia usimamizi dhabiti wa uhifadhi, kushirikiana na jamii, ubunifu wa teknolojia na kutumia askari mahiri tunaleta mabadiliko chanya na matokeo endelevu ya uhifadhi.

Ripoti ya Matokeo 2023

“Mafanikio endelevu ya uhifadhi wa maeneo ya magharibi mwa Serengeti ni matokeo ya pande mbili ya kulinda wanyamapori na kuboresha maisha ya jamii za pembezoni mwa maeneo haya.”

Pakua

Miradi muhimu

Mafanikio ya kazi za uhifadhi na kuboresha maisha ya jamii za pembezoni zinazofanywa na Grumeti Fund hutegemea uhisani wa wafadhili. Mchango wako utasaidia kuendelea kuhifadhi maeneo haya muhimu ya Ikolojia ya Serengeti na kusaiidia maendeleo ya jamii za pembezoni.

Changia

Habari Mpya

Fuatilia baadhi ya nyakati zetu nzuri zaidi za nyuma ya pazia na endelea kuhabarika na Habari zetu mpya na baadhi ya makala zenye taarifa kedekede hapa chini.

  • Safari ya Mafanikio

    Rashidi Nyarata, mkazi wa jamii inayozunguka eneo la hifadhi la Grumeti, ana hadithi ya kipekee ya uvumilivu na mabadiliko. Kabla ya mwaka 2019, maisha ya Rashidi yaligubikwa na changamoto. Akipambana na ulevi na kushindwa kupata kipato cha kutosha, mustakabali wake haukuwa na uhakika. Hata hivyo,......

  • Miguu kwenye Doria: Kitengo cha Mbwa Kazini

    Ndani ya mwezi uliopita kitengo chetu cha mbwa kimekuwa kikifanya kazi kwa bidii kwa ushirikiano na Kikundi cha Operesheni Maalum (SOG) na washirika wetu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) ili kulinda wanyamapori ndani ya mapori  yetu ya akiba. Mwezi huu umeonekana kuongezeka......

  • Kulinda Eneo la Hifadhi ya Grumeti: Juhudi Zisizokoma za Timu ya Usimamizi wa Uhifadhi

    Timu ya Usimamizi wa Uhifadhi (CM) ya  Grumeti Fund inatekeleza jukumu muhimu katika kuhakikisha afya na ustawi wa mfumo wa ikolojia wa mapori ya akiba  ya Grumeti. Timu hii yenye bidii inafanya kazi bila kuchoka kudumisha usawa wa kiasili wa eneo hili , kuhakikisha linaendelea......

Makala zaidi

Washirika wakuu

                  

Tafadhali tambua kuwa unahamishwa kwenda kwenye kurasa ya Shirika la Uhifadhi na Jamii za Kiafrika, Inc.

Nchini Marekani, Grumeti Fund ni mradi unaosaidiwa-kifedha na Shirika la Uhifadhi na jamii za Kiafrika, Inc. (“ACCF”), shirika la kimsaada 501(c) (3). Michango yenye kutozwa kodi kwa ACCF hutolowa kwa Grumeti Fund kusaidia kazi yetu.

Bonyeza hapa kuchangia