Grumeti Fund

Grumeti Fund ni Shirika lisilo la faida linalochangia kuhifadhi Ikolojia ya
Serengeti kwa vizazi vijavyo.

TAZAMA VIDEO KAMILI

Kazi zetu

Sehemu nyingi ulimwenguni zinapoendelea kuharibika kutokana na ongezeko kubwa la watu, Grumeti Fund kwa kushirikiana na washirika wetu wa Tanzania inajizatiti katika kuhifadhi ekari 350,000 za eneo la Magharibi mwa Serengeti zilizopuuzwa hapo awali. Kupitia usimamizi dhabiti wa uhifadhi, kushirikiana na jamii, ubunifu wa teknolojia na kutumia askari mahiri tunaleta mabadiliko chanya na matokeo endelevu ya uhifadhi.

front

Ripoti ya Matokeo 2021

“Mafanikio endelevu ya uhifadhi wa maeneo ya magharibi mwa Serengeti ni matokeo ya pande mbili ya kulinda wanyamapori na kuboresha maisha ya jamii za pembezoni mwa maeneo haya.”

Pakua

Miradi muhimu

Mafanikio ya kazi za uhifadhi na kuboresha maisha ya jamii za pembezoni zinazofanywa na Grumeti Fund hutegemea uhisani wa wafadhili. Mchango wako utasaidia kuendelea kuhifadhi maeneo haya muhimu ya Ikolojia ya Serengeti na kusaiidia maendeleo ya jamii za pembezoni.

Changia

Habari Mpya

Fuatilia baadhi ya nyakati zetu nzuri zaidi za nyuma ya pazia na endelea kuhabarika na Habari zetu mpya na baadhi ya makala zenye taarifa kedekede hapa chini.

  • Kufungua Fursa: Davis Merinyo’s na Mafunzo ya Vitendo kazini Grumeti Fund

    Programu ya Mafunzo kazini ya Grumeti Fund inatoa fursa kwa wanafunzi na wahitimu wa vyuo vikuu kupata uzoefu na kukuza stadi zao za kitaalamu katika fani zao. Davis Merinyo ni miongoni mwa wanafunzi waliopata nafasi kwenye programu hii ambaye ameleta mchango mkubwa wakati akishirikiana na......

  • Tafiti Mpya ya George Lohay Imechapishwa

    Kichwa cha Tafiti: Ushahidi wa Jenetiki wa kugawanyika kwa idadi ya Twiga wa Masai waliotenganishwa na Bonde la Gregory nchini Tanzania (linki) Mshiriki mpya wa timu ya RISE, George Lohay, tayari ameanza kujenga njia mpya na kufanya maendeleo ya kuhifadhi wanyamapori wa Afrika. George amekuwa......

  • Progaramu ya Uhisani ya RISE: Kumwangazia Juma Minya

    Mwaka 2019, Grumeti Fund ilianzisha programu yetu ya Utafiti na Ubunifu kwa ajili ya Mfumo wa Ikolojia ya Serengeti (RISE). Programu za RISE huvuka mipaka ya utafiti wa kawaida. Kwa kutumia vipaji na wasomi wenye maono Tanzania na nje ya nchi, RISE inajenga daraja kati......

Makala zaidi

Washirika wakuu

                  

Tafadhali tambua kuwa unahamishwa kwenda kwenye kurasa ya Shirika la Uhifadhi na Jamii za Kiafrika, Inc.

Nchini Marekani, Grumeti Fund ni mradi unaosaidiwa-kifedha na Shirika la Uhifadhi na jamii za Kiafrika, Inc. (“ACCF”), shirika la kimsaada 501(c) (3). Michango yenye kutozwa kodi kwa ACCF hutolowa kwa Grumeti Fund kusaidia kazi yetu.

Bonyeza hapa kuchangia