Tafiti na ufuatiliaji

Ilikuweza kufahamu vizuri mifumo ya kiikolojia katika eneo husika, na kuweza kupima ufanisi wa kazi zetu za kijamii na uhifadhi, tunawekeza kikamilifu kwenye programu za utafiti na ufuatiliaji kwa lengo la kuboresha kumbukumbu za muda mrefu za mabadiliko ya vigezo muhimu.

Timu yetu ya ufuatilia mazingira, kiwango cha kaboni kwenye udongo, mzunguko wa maji, kiwango cha uoto na hali ya spishi, moto, spishi vamizi (wanyama na mimea), idadi ya wanyama wakubwa, spishi kubwa na muhimu za ndege na migogoro ya binadamu na wanyamapori. Programu ya kisasa ya ramani za GIS huwasaidia kuweka alama kwa usahihi kwenye kila kitu kuanzia mioto pori na uvamizi wa mimea vamizi hadi migogoro ya binadamu na wanyamapori na matukio ya ujangiri. Hizi taarifa huongoza maamuzi yetu.

Migogoro ya binadamu na wanyamapori

Kuunganisha taarifa zetu juu ya programu ya uangalizi wa migogoro ya binadamu na wanyamapori na ile ya maafisa wanyamapori wa jamii, tunaongeza uelewa wetu wa visababishi, kina na mtawanyiko wa muda-na-sehemu wa migogoro ya binadamu na wanyamapori. Kwa kuelewa vipindi na jiografia ya migogoro ya binadamu na wanyamapori vizuri, tunaweza kupanga, kushauri na kutekeleza njia bora za kupunguza.

Camera Traps
HEADER

Uangalizi wa wanyamapori

Idara ya Tafiti na Ufuatiliaji imeunda miradi kadhaa inayolenga kupata uelewa wa kina wa mabadiliko ya idadi ya wanyamapori ikijumuisha kiwango na mipaka cha wanyama wawindao na tabia na mienendo ya tembo.

Kamera za kuangalizia mitego

Mtazamo mpana wa ufuatiliaji wa wanyamapori ni kukusudia wanyama wa kati na wakubwa ikiwa ni pamoja na spisi za wanyama wenye kuona usiku ili kuweza kuelewa vizuri mtawanyiko wao katika hifadhi na mabadiliko ya kiwango idadi yao kulingana na muda. Grumeti Fund hufanikisha kazi hii kwa kushirikiana na kitengo cha simba cha chuo kikuu cha Minnesota.

Kuwavisha tembo kola

Huu mradi una sehemu mbili na unakusudia kutengeneza seti ya taarifa ya muda mrefu kuweza kuelewa vizuri mienendo ya tembo na utawanyikaji wao na kama zana ya usimamizi wa kuzuia migogoro ya binadamu na tembo kwa kutuwezesha kuingilia kati na kuzuia tembo wanaotembea kwenda vijijini.

Ufuatiliaji wa spishi muhimu

Kwa kushirikiana na Idara ya uongozaji watalii ya Singita huu mradi huangazia kwa sehemu kubwa idadi na utambuzi wa kanivorasi katika eneo tengefu.

Ushirikiano wa tafiti

Kuweza kukabili masuala na changamoto za kiusimamizi katika kazi zetu, Grumeti Fund inaanzisha ushirikiano na vyuo vikuu mahiri na taasisi za utafiti kuweza kufanya pamoja tafiti muhimu katika kiwango cha uzamili. Mada na dhima za utafiti, kama vile kuelewa vema kupungua kwa kasi kwa idadi ya Korongo kwenye hifadhi, kusemea moja kwa moja mahitaji ya kiusimamizi yanayofahamika na kuimarisha ufanisi.

GRUMETI FUND

Programu ya utambulishaji upya wa wanyamapori

Kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI), Idara ya Utafiti na Ufuatiliaji ya Grumeti Fund ilifanya utafiti wa kina wa maskani na uoto kufahamu ubora wa hifadhi kwa ajili ya utambulishaji mpya wa wanyama aina ya Tandala Mkubwa waliokuwepo hapo awali na sasa hawapo maeneo haya. Idara hii pia ni muhimu kwa upanuzi wa programu ya faru mweusi na mradi mwingine wowote uhusuo utambulishaji mpya wa wanyamapori.

Soma zaidi

Mafanikio

10+
Miaka ya ufuatiliaji wa kina wa taarifa za kiikolijia

7
Ushirikiano wa kitafiti na taasisi zinazoongoza kitaaluma

332
Kamera zilizowekwa

12
Kola za gps zilizowekwa kwa tembo wasumbufu

Key Accomplishments

                  

Tafadhali tambua kuwa unahamishwa kwenda kwenye kurasa ya Shirika la Uhifadhi na Jamii za Kiafrika, Inc.

Nchini Marekani, Grumeti Fund ni mradi unaosaidiwa-kifedha na Shirika la Uhifadhi na jamii za Kiafrika, Inc. (“ACCF”), shirika la kimsaada 501(c) (3). Michango yenye kutozwa kodi kwa ACCF hutolowa kwa Grumeti Fund kusaidia kazi yetu.

Bonyeza hapa kuchangia