Research and Innovation for the Serengeti Ecosystem (RISE)

Kuhusu Sisi

Utafiti na Ubunifu kwa Mfumo wa Serengeti (RISE) ni programu ya utafiti tumizi na kituo, iliyozinduliwa na Grumeti Fund mwaka 2019. RISE inalenga kuendeleza na kusaidia utafiti wenye mwelekeo wa vitendo na suluhisho kwa faida ya watu na wanyamapori wa mfumo wa Serengeti na zaidi. RISE inalenga kuunganisha wanasayansi kutoka Tanzania na ulimwenguni kote, kutoka kwa wanafunzi wa shahada ya uzamili hadi wanasayansi wa karibuni, kufanya kazi kwa ushirikiano katika miradi ya utafiti ambayo kimsingi inahusiana na maswali muhimu katika sayansi ya uhifadhi na kupata suluhu ambazo kwa wakati mmoja ni za ubunifu na za vitendo. RISE inaahidi kuimarisha uwezo wa ndani na kuwekeza katika watu wenye shauku na vipaji ambao wamejitolea kwa uhifadhi na usimamizi wa maeneo ya uhifadhi na rasilimali asilia za Tanzania zinazojulikana ulimwenguni.

Jukumu

Jukumu letu ni kuchangia katika maendeleo ya zana, suluhisho, maarifa, na uwezo wa kukabiliana na changamoto za uhifadhi zinazotukabili wakati huu, ili kuunga mkono maamuzi endelevu yanayonufaisha watu na wanyamapori wa mfumo wa Serengeti na zaidi, wakati tukishirikiana na washirika nchini Tanzania na nje ya nchi.

Tafiti

Kazi zetu za sasa zinajumuisha ekolojia ya mijongeo ya tembo, migogoro kati ya binadamu na tembo, ekolojia ya uzio, mafanikio ya uzazi wa tai, udhibiti wa uharibifu wa mimea ya kigeni, na ekolojia ya kurudisha tena faru weusi. Kazi hii inafanywa kwa ushirikiano na uratibu na watu mbalimbali, vyuo vikuu, na taasisi za serikali. Taasisi muhimu tunazoshirikiana nazo ni pamoja na Chuo Kikuu cha Colorado State, Chuo Kikuu cha Leiden, Taasisi ya Max Planck, Bustani ya Wanyama ya North Carolina, Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, Chuo Kikuu cha Stanford, TAWIRI, Chuo Kikuu cha Glasgow, Chuo Kikuu cha Groningen, na Chuo Kikuu cha Minnesota. Utafiti wote unafanywa kwa idhini ya TAWIRI, COSTECH, TAWA, na TANAPA.

Programu

Tunatoa na kuendesha programu za mafunzo kwa wanafunzi, watafiti wa awali, na wataalamu wa umma na wa kibinafsi katika sekta ya uhifadhi na utafiti. Programu za sasa zinazingatia teknolojia ya uhifadhi (kwa kushirikiana na Fauna and Flora Int’l na WildLabs), njia za kisayansi za ekolojia na sayansi ya kijamii, mawasiliano ya kisayansi (kwa kushirikiana na AfriSOS na Chuo Kikuu cha Leiden), na uchambuzi wa data za nafasi. Tumejizatiti kutumia programu zetu kuendeleza ushiriki na fursa kwa wale ambao wamekuwa kihistoria hawahusishwi katika sekta ya uhifadhi – tunatoa programu maalum kwa wanawake na programu zingine zote zinalenga usawa wa kijinsia.

Women in the Field (WIF)

Women in the Field (WIF) ni programu yetu ya mafunzo ya kipekee – ilizinduliwa mwaka 2019, programu hii inalenga kuunda jukwaa la kuanzia kwa maendeleo ya kizazi kijacho cha wanawake wanasayansi na wahifadhi wa Kitanzania katika mazingira yenye msaada na motisha yanayolenga mafunzo ya ubora wa juu na ujuzi. Katika kipindi cha wiki tatu, tunawapa wanafunzi ujuzi thabiti ambao wanaweza kutumia katika kazi zao na kuwaunganisha washiriki, wataalamu na viongozi wa taasisi kwenye hii sekta. Baada ya programu kukamilika, tunaendelea kuwaunganisha washiriki na fursa katika sekta ya uhifadhi na utafiti na tumejizatiti kuwasaidia washiriki wanapoendelea katika kazi na elimu zao. Programu ya WIF imekuwa mwongozo wa kupitisha programu kama hizo nchini Msumbiji na Kenya. Programu ya WIF isingewezekana bila mchango wa walimu kutoka Southern Tanzania Elephant Program, Lion Landscapes, Chuo Kikuu cha Glasgow, na wahitimu wa programu ambao wanarudi kushiriki ujuzi wao.

Miundombinu yetu

Mwaka 2020, tulikamilisha mchakato wa ujenzi wa kituo cha utafiti cha kisasa. Kituo hiki kinatoa nafasi ya ofisi iliyoundwa kwa umakini na kutoa fursa kwa wanasayansi wa Kitanzania na kimataifa kuweza sio tu kufanya kazi, bali pia kujitosa kwenye mazingira ambayo ni kitovu cha utafiti wao. Kituo hicho kinatoa nafasi ya kufanya kazi kwa pamoja, vyumba vya mikutano, chumba kikubwa cha mkutano kinachoweza kuchukua hadi watu 30, nafasi ya kujiandaa na kazi, na nafasi ya kutosha ya kuhifadhi vitu.

Malazi kamili ya hema yanapatikana kwa watu 12 kwa kiwango cha $10 kwa mtu kwa siku. Hema tatu zilizojengwa kwenye majukwaa yaliyopangwa vizuri, kila hema imegawanywa katika nafasi mbili tofauti zilizo na vitanda viwili kila moja na nafasi ya kuhifadhi vitu. Kila hema ina umeme, choo binafsi, na bafu (ikiwa ni pamoja na maji ya moto). Sehemu ya chakula ina jikoni kamili na viti vya kutosha hadi watu 25. Wafanyakazi wa jikoni hutoa milo mitatu yenye Ladha nzuri  kwa kutumia viungo vya kitanzania.

Miundombinu yetu ilibuniwa kwa kuzingatia uhifadhi wa mazingira – miundombinu yote inatumia nishati ya jua na hutegemea kabisa maji ya mvua yaliyokusanywa kutoka kwenye paa la kituo chetu cha utafiti. Majengo yamejengwa ili kutumia vema mwanga wa asili, baridi, na uingizaji hewa. Vifaa viliagizwa kwa kuzingatia haya, na ni pamoja na mbao zilizothibitishwa na FSC, sakafu iliyotengenezwa kutoka plastiki iliyosindikwa tena, na msingi  uliowekwa kwa umakini wakati wa uchimbaji na kutumika tena kwa kuta za kuzuia za zamani. Mazingira ya ndani yaliyobuniwa vizuri hujumuisha mafundi wa Tanzania ikiwa ni pamoja na Dunia Designs, Shanga, Green Room, na Starfish pottery. Tunajivunia kuwa karibu vifaa vyote vingine vilitengenezwa kwenye tovuti na timu za mafundi wa ujenzi wa Grumeti.

Watafiti Tunaowatazamia

Watu wote wanaofanya utafiti nchini Tanzania lazima wapate kibali cha utafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI), Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), na mamlaka husika za usimamizi wa maeneo ya hifadhi inayosimamia maeneo ambapo utafiti utafanyika (TAWA, TANAPA). Watafiti wa kigeni pia watahitaji kupata Kibali cha Makazi cha Daraja C. Watafiti wapya wanapaswa kuzingatia muda wa hadi miezi 6 ili mapendekezo yao yafanyiwe ukaguzi na kibali kupokelewa.

RISE haitoi idhini wala ruhusa za utafiti.
Tupo tayari kujadili mchakato wa kupata kibali kwa wale wanaoanza kufanya utafiti unaohusiana na wanyamapori nchini Tanzania.
Ikiwa una nia ya kushirikiana na RISE, tafadhali tuma barua pepe. Tunatoa kipaumbele kwa ushirikiano unaolingana na kazi yetu iliyopo na/au vipaumbele vya utafiti wa Grumeti Fund.

Kulingana na nafasi, malazi na miundombina vya RISE vinapatikana kwa watafiti wowote wanaofanya kazi katika mandhari ya Ikorongo-Grumeti na jamii za pembezoni. Kipaumbele kinatolewa kwa wanaoshirikiana na wanafunzi wa shahada ya uzamili ambao tunawasaidia. Tuma barua pepe kuulizia ratiba na upatikanaji.

Wasiliana Nasi

Kwa maswali kuhusu ushirikiano wa utafiti na/au programu za kushirikiana, na malazi na/au msaada wa logistiki kwenye eneo, tafadhali wasiliana nasi kupitia RISE@grumetifund.org

Kristen Denninger Snyder, PhD

Mwanasayansi Kiongozi

George Lohay, Ph.D.

Mwanasayansi wa Utafiti – RISE

Victoria Mkessa

Mratibu wa Programu

Teddy John

Mpishi

Emmy John

Mfanya usafi ndani

Wanafunzi wa sasa

Michael Kimaro, Chuo Kikuu cha Groningen, PhD
“Managing human-wildlife conflict along hard boundaries of African protected areas through fencing”
Vainess Laizer, Chuo cha Kilimo Sokoine, MSc
“Breeding success, breeding population status, and habitat preferences of the critically endangered white-backed vulture (Gyps africanus) in Western Serengeti, Northern Tanzania”
Juma Minya, Chuo Kikuu cha Glasgow, MSc
“Assessment of age and sex structures of elephants in western Serengeti”
Exavery Kigosi, Chuo Kikuu cha Leiden, PhD
“Impacts of Invasive Alien Plants in the Western Serengeti”

Wanafunzi waliopita.

Loyce Majige, Chuo Kikuu cha Glasgow, MSc
“Impact of electric fencing on elephant (Loxodonta africana) movement behavior along a protected area boundary of the Serengeti ecosystem”

Washiriki waliopita kwenye programu ya Women in the Field

Hadi mwaka 2022, wanawake thelathini na nne walishiriki katika programu hii. Wanawake kumi na tatu walijiunganisha na fursa za kazi au mafunzo ya vitendo kutokana na uhusiano ulioundwa wakati wa programu, na wanawake saba wamefanikiwa kupata fursa za masomo ya shahada ya uzamili zilizofadhiliwa kila kitu kutokana na msaada wa wafanyakazi kwenye programu hii na walimu wageni.

Washiriki

WIF 2019

Kim Lim – Southern Tanzania Elephant Program
Loyce Majige – Southern Tanzania Elephant Program
Magreth Victor – Eastern Arc Mountains Conservation Endowment Fund
Vainess Laizer – Sokoine University of Agriculture (MSc)

WIF 2020

Leena Lulandala – Camp and research administrator, Asilia Africa
Nyasatu Mkaka – Lion Landscapes and University of Oxford (Postgraduate Diploma)
Plakizia Msalilwa – Oikos, University of Glasgow (MSc)
Yamat Lengai – African People and Wildlife

WIF 2021

Angel Masaki – Univerity of Jagiellonian, Poland (MSc)
Catherine Kimario – Intern, Southern Tanzania Elephant Program
Cephuline Makungu – Seeking opportunities
Christina Mgonja – Field Assistant, Southern Tanzania Elephant Program
Damfa Hassan – Seeking opportunities
Doreen Mungure – Seeking opportunities
Doreen Olomi – TAWA
Evaline Munisi –TAWIRI
Georgina Minja – Seeking opportunities
Huruma Mbugi – Lion Landscapes
Jesca Mchomvu – Tanzania Wildebeest Research Project, TAWIRI
Lucia Romward – Tutorial Assistant, University of Dar es Salaam
Lollian Kosyando – University of Glasgow (MSc)
Maria Matata – Wildlife Officer intern, Mwanza Airport

WIF 2022

Agnes Ngao – Forest Officer, Sokoine University of Agriculture
Beatrice Msenga – Nelson Mandela African Institute of Science and Technology (MSc)
Beatrice Modest – Wildlife Officer, Hanang District Council
Debora Magesa – Assistant Lecturer, Sokoine University of Agriculture
Elizabeth Masatu – Intern, Southern Tanzania Elephant Program
Ellen Ponsian – TAWIRI
Eva Johnson – EDGE Fellow, Zoological Society London
Happyness Jackson – Landscape and Conservation Mentors Organization (LCMO)
Huruma David – Intern, Southern Tanzania Elephant Program
Irene James – Sokoine University of Agriculture (MSc)
Providence Nyenza – Forest Officer, Tanzania Forestry Services
Tatu Shaibu – Seeking opportunities

Walimu waliopita na wa sasa

Aidat Mugula, MD, MSc
Ana Grau, MSc – Lion Landscapes
Anna Czupryna, PhD – Chuo Kikuu cha Glasgow
Anna Estes, PhD – Carleton College
Catherine Getige, MSc – Wizara ya Afya
Emma Impink – Southern Tanzania Elephant Program
Evaline Munisi, MSc – TAWIRI
Josephine Smit, PhD – Southern Tanzania Elephant Program
Plakizia Msalilwa – Oikos, Chuo Kikuu cha Glasgow
Sarah Cleaveland, PhD – Chuo Kikuu cha Glasgow
Vainess Laizer – Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine 

                  

Tafadhali tambua kuwa unahamishwa kwenda kwenye kurasa ya Shirika la Uhifadhi na Jamii za Kiafrika, Inc.

Nchini Marekani, Grumeti Fund ni mradi unaosaidiwa-kifedha na Shirika la Uhifadhi na jamii za Kiafrika, Inc. (“ACCF”), shirika la kimsaada 501(c) (3). Michango yenye kutozwa kodi kwa ACCF hutolowa kwa Grumeti Fund kusaidia kazi yetu.

Bonyeza hapa kuchangia