Miguu kwenye Doria: Kitengo cha Mbwa Kazini

Ndani ya mwezi uliopita kitengo chetu cha mbwa kimekuwa kikifanya kazi kwa bidii kwa ushirikiano na Kikundi cha Operesheni Maalum (SOG) na washirika wetu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) ili kulinda wanyamapori ndani ya mapori  yetu ya akiba. Mwezi huu umeonekana kuongezeka kwa vitendo vya ujangili kutokana na wingi wa nyumbu wanaohama katika eneo hilo.

Mwezi Julai pekee kitengo cha mbwa kilishiriki katika operesheni 14 za pamoja na kuimarisha mikakati yetu ya kupambana na ujangili kwa kuchanganya utaalamu wa skauti wetu na uwezo mkubwa wa kufuatilia wa mbwa wetu waliofunzwa.

Tukio moja la tarehe 2 Agosti lilionyesha uwezo mkubwa wa kitengo chetu cha mbwa. Wakati wa doria ya asubuhi askari wetu wa wanyama pori na askari wa TAWA walikutana na kundi la majangili wakijaribu kukimbia kwa pikipiki. Mwitikio wa haraka wa timu hizo uliwalazimu majangili hao kuachana na pikipiki zao na kutoroka kwa miguu. Maskauti wetu waliwaita mara moja kitengo cha mbwa na Rada mmoja wa mbwa wetu stadi akatumwa.

Utendaji wa rada ulikuwa wa kipekee kwani alifuatilia nyayo za wawindaji haramu kwa zaidi ya kilomita saba na kufikisha timu yetu kwenye Kijiji Jirani cha Motukeri. Ingawa wawindaji haramu waliweza kujichanganya na wanakijiji na hivyo kuzuia mchakato kuendelea, utaalam wa Rada ulikuwa wenye msaada mkubwa.

Kitengo chetu cha mbwa sio tu kikundi cha mbwa wanaofanya kazi; bali ni wanachama muhimu wa timu yetu ya uhifadhi. Tunahakikisha wanapata matunzo ya hali ya juu, ikijumuisha mafunzo stahiki ya mara kwa mara na uchunguzi wa afya wa mara kwa mara. Hivi majuzi tuliwapatia chanjo dhidi ya magonjwa yanayoenezwa na wadudu, hatua muhimu ya kuwafanya kuwa na afya njema.

Tunapotafakari mwezi uliopita, tunajivunia na kushukuru kwa kazi kubwa iliyofanywa na Rada na kitengo kizima cha mbwa. Tunaendelea kujitolea kuwaunga mkono kwa kila njia iwezekanavyo kuhakikisha wanaendelea kuchukua jukumu muhimu kwenye mafanikio yetu ya uhifadhi.

Ili kusaidia kitengo chetu cha mbwa tafadhali bofya hapa.

                  

Tafadhali tambua kuwa unahamishwa kwenda kwenye kurasa ya Shirika la Uhifadhi na Jamii za Kiafrika, Inc.

Nchini Marekani, Grumeti Fund ni mradi unaosaidiwa-kifedha na Shirika la Uhifadhi na jamii za Kiafrika, Inc. (“ACCF”), shirika la kimsaada 501(c) (3). Michango yenye kutozwa kodi kwa ACCF hutolowa kwa Grumeti Fund kusaidia kazi yetu.

Bonyeza hapa kuchangia