Mnyumbuliko wa visababishi katika uharibifu unaosababishwa na wanyamapori unahitaji mikakati mahusus  kwa kila spishi ili kuipunguza katika Magharibi mwa Serengeti, Tanzania.

Waandishi

Kristen Denninger Snyder

Kate M. Tiedeman

Brendan J. Barrett

Mackiana Kibwe

Robert J. Hijmans

George Wittemeyer

Muhtasari

Katika maeneo yanayotegemea kilimo ambayo yamechanganyika na maeneo ya porini, uharibifu wa mazao na kuuwawa kwa mifugo kunakosababishwa na wanyamapori unatishia maisha ya vijijini na kudhoofisha juhudi za uhifadhi. Kujua spishi, shughuli za kibinadamu, na vipengele vya mandhari vinavyohusiana na hasara zinazosababishwa na wanyamapori ni muhimu kwa ajili ya kukuza njia bora za kupunguza madhara hayo. Ili kuelewa vyema sababu za uharibifu unaosababishwa na wanyamapori, tulifanya utafiti kwenye kaya 419 magharibi mwa Serengeti, Tanzania kuhusu namna ya uendeshaji wa shughuli za kilimo na hasara zinazosababishwa na wanyamapori. Kwa kutumia mfumo wa kutoa uhakika wa kihusishi na mifano ya Bayes, tukichunguza mchango wa tabia za mazingira na kaya kwa uharibifu unaosababishwa na spishi mbalimbali za wanyamapori. Hasara ya mazao kutokana na tembo ilikuwa aina ya uharibifu ulioenea zaidi; hasara ya mazao kutokana na nyani na tumbili ilikuwa haionekani sana. Uwindaji wa mifugo na fisi ulikuwa mkubwa na wa kawaida, wakati uwindaji na simba ulikuwa nadra na uliotokea maeneo machache. Wengi wa washiriki waliona wanyamapori kama tishio kubwa kwa uzalishaji wa mazao, wakati ufanisi wa uzazi na sababu za mazingira zilionekana kuwa tishio kubwa kuliko wanyamapori kwa mifugo. Hatari ya uharibifu wa mazao na mifugo ilihusiana kwa kawaida na kuingiliwa kwa binadamu, na ilihusiano chanya na ukubwa wa shamba na kundi la mifugo. Mchango wa vipengele vingine, ikiwa ni pamoja na upandaji wa miti, mteremko, na umbali na makazi, ulitofautiana kulingana na aina ya uharibifu na spishi. Matokeo yetu yanaashiria kuwa kupanga matumizi ya ardhi kunaweza kuwa njia ya jumla ya kupunguza uharibifu wa wanyamapori, lakini tofauti katika sababu zinazochochea uharibifu, kiwango cha uharibifu, hali ya uhifadhi, na uvumilivu wa hasara zinaonyesha kuwa njia za kupunguza madhara kwa kuzingatia spishi zinahitajika. Tathmini za spishi mbalimbali hutoa ufahamu mpana katika uhusiano kati ya binadamu na wanyamapori na zinaweza kusaidia katika kutambua na kuweka kipaumbele cha hatua za kupunguza madhara. Soma makala kamili.

                  

Tafadhali tambua kuwa unahamishwa kwenda kwenye kurasa ya Shirika la Uhifadhi na Jamii za Kiafrika, Inc.

Nchini Marekani, Grumeti Fund ni mradi unaosaidiwa-kifedha na Shirika la Uhifadhi na jamii za Kiafrika, Inc. (“ACCF”), shirika la kimsaada 501(c) (3). Michango yenye kutozwa kodi kwa ACCF hutolowa kwa Grumeti Fund kusaidia kazi yetu.

Bonyeza hapa kuchangia