Kulinda Eneo la Hifadhi ya Grumeti: Juhudi Zisizokoma za Timu ya Usimamizi wa Uhifadhi

Timu ya Usimamizi wa Uhifadhi (CM) ya  Grumeti Fund inatekeleza jukumu muhimu katika kuhakikisha afya na ustawi wa mfumo wa ikolojia wa mapori ya akiba  ya Grumeti. Timu hii yenye bidii inafanya kazi bila kuchoka kudumisha usawa wa kiasili wa eneo hili , kuhakikisha linaendelea kufanya kazi na kustawi kwa ajili ya wageni ambao ni binadamu na wanyama pori wanaoishi humo.

Dhamira ya timu ya CM si rahisi. Kila siku, wanakabiliana na changamoto kubwa katika juhudi zao za kulinda wanyama  pori na maskani yao ndani ya eneo la hifadhi. Miongoni mwa changamoto hizi ni kuwepo kwa uwindaji haramu, au ujangili, ni miongoni mwa  masuala yanayohitaji muitikio wa haraka  na yenye kuhuzunisha  zaidi. Ujangili ni tishio kubwa kwa maeneo mengi ya uhifadhi  barani Afrika, huku ujangili wa mitego ya waya ukiwa moja ya mbinu za kawaida na mbaya zaidi zinazoonekana mbugani. .

Mitego ya waya, iliyoundwa kunasa wanyama kwa kuwakaba wanapotembea, ni zana mbaya  ambazo mara nyingi utengenezwa  kwa waya  kama vile  za matairi ya magari. Mitego hii huwekwa kando ya njia zinazotumiwa sana na wanyama wakubwa kama vile nyumbu na pundamilia, au kuwekwa kwenye miti ili kunasa twiga. Wawindaji haramu wakati mwingine huunda njia za bandia ili kulazimisha wanyama kupita kwenye mitego hiyo.

Malengo makuu ya ujangili wa mitego ni spishi za “nyama za porini,” ikiwa ni pamoja na nyumbu, nyati, twiga, na pundamilia, ambazo huuzwa katika jamii za karibu au maeneo yenye mahitaji makubwa ya nyama pori. Hata hivyo, mitego haiwezi kuchagua na inaweza kumnasa mnyama yeyote anayepita njia hiyo, ikiwa ni pamoja na tembo, simba, na fisi. Ingawa wanyama wakubwa wanaweza kujinasua kwenye mitego, mara nyingi wanapata majeraha makubwa kwani  waya unakata ndani ya ngozi , kusababisha maumivu makali, maambukizi, na wakati mwingine kifo.

Ili kupambana na vitendo hivi vya kikatili, timu ya CM ya Grumeti inashirikiana na mamlaka za wanyamapori  kama vile TAWIRI, TANAPA, na TAWA. Pamoja, wanajitahidi kuzuia vifo vya kikatili  vya wanyama kwa kuondoa mitego na kuimarisha juhudi za utekelezaji wa sheria.

 Grumeti Fund imejitolea kupunguza uwindaji haramu ndani ya eneo la hifadhi ili kuboresha afya ya mfumo wa ikolojia wa Serengeti na wakazi wake. Mkakati wao unajumuisha sio tu utekelezaji wa sheria bali pia elimu na utoaji wa fursa za ajira. Wawindaji wengi haramu hugeukia uwindaji haramu ili kujikimu wao na familia zao. Kwa kuhusisha jamii za wenyeji katika juhudi za uhifadhi na kutoa njia mbadala za maisha,  Grumeti Fund inalenga kutengeneza suluhisho endelevu zinazowanufaisha jamii za wenyeji  na malengo ya uhifadhi.

Kupitia juhudi hizi za pamoja,  Grumeti Fund na timu yake ya CM wanatarajia kukuza mazingira salama kwa wanyamapori na kuhakikisha ustawi unaoendelea wa mfumo wa ikolojia wa Eneo la Hifadhi ya Grumeti.

                  

Tafadhali tambua kuwa unahamishwa kwenda kwenye kurasa ya Shirika la Uhifadhi na Jamii za Kiafrika, Inc.

Nchini Marekani, Grumeti Fund ni mradi unaosaidiwa-kifedha na Shirika la Uhifadhi na jamii za Kiafrika, Inc. (“ACCF”), shirika la kimsaada 501(c) (3). Michango yenye kutozwa kodi kwa ACCF hutolowa kwa Grumeti Fund kusaidia kazi yetu.

Bonyeza hapa kuchangia